• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watoto Mazingira hatarishi jijini Dodoma wakutana na Waziri Gwajima

Imewekwa tarehe: January 19th, 2022

WATOTO waishio katika mazingira magumu kwenye Jiji la Dodoma wamemueleza Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, (Mb), madhila wanayokumbana nayo katika mitaa wanayoishi huku wakiiomba Serikali iweze kuwanusuru na maisha hayo kwa kuwa siyo kusudi lao kuishi hivyo.

Hayo yamejiri jana Januari, 17, 2022 Waziri huyo alipoongoza jopo la wataalamu wa Wizara hiyo, Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenda mitaani wanakoishi watoto hao kwa ajili ya kuzungumza nao na kujifunza toka kwao jinsi gani Serikali inaweza kuwabadilishia maisha yao yawe na ustawi zaidi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti watoto hao walioweza kufikiwa, walisimulia madhila na changamoto wanazopitia wakiwa katika mitaa mbalimbali ya Jiji la DODOMA.

“Mhe. Waziri, sisi watoto tuishio katika mazingira ya mitaani tunapitia madhila mengi sana, tunalazimika kutumia vilevi, kujifunza mambo mengi mabaya pia tunafanyiwa mambo mabaya na tunalazimika kuwa watu wasio wema ili tuishi na matokeo yake tunabaguliwa na kutengwa na jamii” alisema mmoja wa watoto ambaye jina lake limehifadhiwa kwa sababu za kimaadili.

Vilevile, mtoto huyo, alisema wapo baadhi yao wamekuwa wakipitia ukatili wa kupigwa na wenzao wanaowazidi umri, wapo wanaofanyiwa ukatili wa kingono na kuambukizwa magonjwa na kupata maradhi ambayo mwisho wa siku yameondoa uhai kwenye umri mdogo.

Waziri Dkt Gwajima, akizungumza na Watoto hao, aliwaambia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuboresha ustawi wa watoto na ameunda Wizara mpya ambayo pamoja na mambo mengine itasimamia maendeleo na ustawi wa makundi maalumu ikiwemo watoto kwa ujumla wake.

Hivyo, ziara hiyo ya kujifunza huu ni mwanzo wa safari ya kuwaondoa watoto wanaoishi mitaani, wakaishi maisha salama na yenye ustawi hivyo wananchi na watendaji toeni ushirikiano kwani ufumbuzi wa jambo hili utatokana na wanajamii wenyewe.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula, alisema tayari ameanza kuratibu ushirikiano na makatibu wakuu wa Wizara zingine ili watoe ushirikiano kwenye operesheni hii kubwa ya kuwarejesha watoto wa mitaani kwenye maisha yenye ustawi na atasimamia jambo hili kwa ushirikiano na wadau wengine wote.

Kwa upande wake Kaspar Kaspar Muya, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu amesema, ofisi hiyo iko tayari kuratibu ushirikishwaji wa wizara na Sekta zote ili jambo hili lifanikiwe kama ilivyokusudiwa kwenye Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA, 2017/18-2021/22) na ILANI ya Uchaguzi Mkuu CCM, 2020-2025.

Kama sehemu ya mpango wa haraka, Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu imeanza kuratibu kuwezesha watoto waishio kwenye mazingira magumu ya mitaani wanarejea kwenye maisha yenye ustawi ili wakiwa watu wazima waweze kuchangia maendeleo ya taifa kwa tija.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatma Mganga akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo amesema, Mkoa upo tayari kushirikiana na wadau wote kusimamia utekelezaji wa zoezi hilo kwa ufanisi.

Ziara hiyo imefanikisha kuwarejesha watoto 14 kwenye makao ya watoto na uratibu unaendelea mkoani Dodoma na utaendelea mikoa yote.

Matangazo

  • Tangazo kuhusu zoezi la Anuani za Makazi na Postikodi April 30, 2022
  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) 2022 April 28, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye USAILI WA MAHOJIANO kwa nafasi za Kazi ya Kukusanya Taarifa za Anwani za Makazi na Postikodi March 04, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili kwa nafasi za Kazi ya Kukusanya Taarifa za Anwani za Makazi na Postikodi February 28, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Serikali kujenga 'Sports and Arts Arena' Dodoma na Dar

    May 24, 2022
  • Rais Samia ziarani nchini Ghana

    May 23, 2022
  • Wakulima Milioni 1 kunufaika na programu ya mkopo wa pembejeo na soko la mazao

    May 20, 2022
  • Tanzania yafikia lengo uwekaji wa Anwani za Makazi - Waziri Nape

    May 20, 2022
  • Angalia zote

Video

DC Shekimweri awakumbusha wakazi Mtumba kutumia vema fedha za fidia
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    3 CDA Street

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.