• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bajeti ijayo gumzo, ni Bilioni 180

Imewekwa tarehe: March 1st, 2019

BAJETI ya Shilingi Bilioni 180 ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliyopitishwa na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo jana kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri kwa Mwaka ujao wa Fedha imesisimua wajumbe wa Baraza hilo na Wananchi wengine kwani imelenga kumaliza kabisa baadhi ya changamoto ikiwemo zilizopo kwenye Sekta ya Elimu ambayo pekee imetengewa zaidi ya Shilingi Bilioni nane.

Katika Mkutano wa Baraza hilo uliofanyika jana katika ukumbi wa Jiji hilo, Baraza limepitisha bajeti hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Godwin Kunambi aliwasilisha Bajeti nzima mbele wajumbe wa Baraza hilo lenye Madiwani 60.

Kunambi alisema bajeti ya Makusanyo yanayotokana na vyanzo vya ndani vya Halmashauri hiyo yanatarajiwa kuwa Shilingi Bilioni 72, ikiwa imeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 68 za Mwaka huu unaondelea.

“Mheshimiwa Mwenyekiti na wajumbe, tukiangalia makusanyo yetu ya ndani kwa bajeti ya Mwaka tulionao sasa ni Bilioni 68, lakini kwa Mwaka ujao tanatarajia kukusanya takribani Bilioni 72 hivyo kuna ongeza la Shilingi Bilioni tano” alisema Kunambi.

Alisema moja ya vipaumbele katika Mpango wa Bajeti hiyo ni kuboresha Sekta ya Elimu ambapo jumla ya Shilingi Bilioni nane zimetengwa.

Mkurugenzi Kunambi alisema Halmashauri anayoiongoza inakusudia kujitegemea na kujiendesha yenyewe kwa asilimia 100 kuanzia Mwaka 2021/2022 ambapo itaachana kabisa na kutegemea ruzuku kutoka Serikali Kuu.

“Tunaposema Halmashauri kujitegemea na kujiendesha yenyewe maana yake ni kwamba tutatekeleza miradi ya Maendeleo katika Kata zetu kwa Fedha za ndani, tutalipa Mishahara ya watumishi wetu wote kwa Fedha za ndani, pamoja na kulipa stahiki mbalimbali za Watumishi…tunakusudia kufikia hatua hii” alifafanua.

Wakichangia hoja hiyo, baadhi ya wajumbe wa Baraza la Halmashauri hiyo wakiongozwa na Mstahiki Meya Profesa Davis Mwamfupe walielezea kufurahishwa kwao na vipaumbele na ukubwa Mpango na Bajeti hiyo kwani wanaamini utaharakisha maendeleo kwa Wananchi wanaoowaongoza.

Mbunge wa Jimbo la Dodoma ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu Anthony Mavunde alisema Bajeti iliyopitishwa inagusa maisha na itaboresha Sekta muhimu ikiwemo Elimu, Afya, na Maji.

“Bajeti hii kwenye Elimu pekeake imetengwa zaidi ya Bilioni nane na hata ukiangalia kwenye Sekta ya Afya kiasi kilichotengwa ni Bilioni Mbili ambacho ni kiasi kikubwa sana …hii itasaidia kujibu kwa vitendo hoja za matumizi ya makusanyo makubwa tunayoyakusanya…hii ni bajeti ambaye kila anayeipenda Dodoma atakubali kuwa ni nzuri” alisema Mavunde.

Mavunde alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndiyo ya kwanza nchini kutenga kiasi kikubwa cha Fedha kwa ajili ya kuwezesha Makundi Maalum ikiwemo watu wenye ulemavu ambao katika Bajeti hiyo wametengewa Shilingi Bilioni 3.3 ambazo zikitolewa kwa walengwa Halmashauri itakuwa imefanya jambo kubwa la kupigiwa mfano.

“Mheshimiwa Mwenyekiti mimi hili ni eneo langu la kazi kule Serikalini na nafahamu changamoto ni kubwa kwenye uwezeshaji, tukienda katika kumbukumbu sisi tutakuwa Halmashauri ya kwanza nchi nzima ambaye tumetenga Fedha nyingi katika makundi haya maalum” alisema Mavunde.

Kwa upande wake Mstahiki Meya Prof. Mwamfupe (Pichani juu) alisema bajeti ya hiyo ni yenye kuacha alama kwani haijawahi kutokea siku za nyuman na kwamba wamefikia hatua hiyo kutokana na juhudi na uzalendo wa Wanadodoma wote.

Alisema Jiji la Dodoma linatakiwa kuwa la mfano ili kuunga mkono juhudi kubwa za Seriikali katika utoaji wa huduma za Kijamii na kwamba ushirikiano na uzalendo kwa wadau ndiyo silaha pekee.

Naye Anselem Kutika ambaye ni Dwani wa Kata ya Kikuyu Kusini alisema anaunga mkono bajeti hiyo kwani haijawahi kutokea huku akitoa pongezi kwa wataalam wote wa Jiji wakiongozwa na Mkurugenzi Kunambi.

“Mheshimiwa Mwenyekiti kabla ya yote nianze kwa kusema kuwa, kwa niaba ya Wananchi ya Kikuyu Kusini naunga mkono bajeti hii kwa asilimia 100…hii ni bajeti ya Wananchi kwani imegusa maisha yao” alisema Kutika wakati akichangia hoja hiyo ya Bajeti.

Bajeti iliyopitishwa na Baraza hilo jana inatarajiwa kuendelea kujadiliwa katika ngazi mbalimbali za juu kabla ya kuanza kutumika mapema Mwezi Julai Mwaka huu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.