• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wadau wa Nyuki watakiwa kuanzisha soko kubwa Dodoma

Imewekwa tarehe: May 20th, 2019

WADAU wa Nyuki wameshauriwa kufungua duka la mazao ya Nyuki Jijini Dodoma ili kuongeza wigo wa kujitangaza na urahisi wa upatikanaji wa asali.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda alipokuwa akifunga maadhimisho ya siku ya Nyuki duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini hapa leo.

“Dodoma tulishakubaliana kufanya mkutano wa wadau wa ufugaji Nyuki, natamani Dodoma tupate eneo ambalo litakuwa ni duka la asali kwa mkoa wa Dodoma…lazima wadau wa asali tukae eneo linaloonekana ili tuuze asali” alisema.

Waziri Mkuu huyo Mstaafu alisema kuwa, kufunguliwa kwa duka la uuzaji asali kutawasaidia wauzaji walio maeneo ya pembezoni kufahamika na bidhaa zao kuuzika kwa urahisi.

Akiongelea umuhimu wa Nyuki, alisema mazao ya nyuki ni chakula, malighafi za viwandani na dawa na kwamba fursa kwa Watanzania ni kubwa kupitia ufugaji nyuki nchini.

“Tanzania ina uwezo wa kuzalisha tani 138,000 za asali na tani 9,200 za nta kwa Mwaka, lakini uzalishaji wa sasa ni tani 4,800 za asali na tani 324 za nta,hivyo fursa bado ni kubwa” alisema Pinda.

Awali, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala alisema kuwa utamaduni wa kufuga Nyuki umepungua sana hivyo msukumo unahitajika na kwamba Serikali imedhamiria kuanzisha chama cha ushirika cha wafugaji nyuki ambacho kitaanza na Mikoa 10 katika Mwaka huu.

Alisema kuwa, katika Mikoa hiyo, kila Wilaya itakuwa na kiwanda cha kuchakata mazao asali huku akidai kuwa changamoto kubwa inayotarajiwa ni kiwango kidogo cha asali kinachozalishwa na wadau.

Siku ya Nyuki duniani ni azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kuwa tarehe 20 Mei, kila mwaka ni siku ya Nyuki duniani kutokana na umuhimu wao katika kuhakikisha ekolojia inakuwa endelevu.

Matangazo

  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 - Awamu ya Pili February 19, 2021
  • Tangazo la Mnada wa Hadhara February 15, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha Nne, cha Pili na Darasa la Nne 2020 haya hapa January 15, 2021
  • Zoezi la upandaji miti watumishi wote January 15, 2021
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Msigwa akabidhiwa ofisi, asisitiza uzalengo kwa Wanahabari

    April 16, 2021
  • RC Mahenge ataka ushirikiano mkataba wa lishe, Wakurugenzi watenge fedha

    April 16, 2021
  • Matumizi ya Mitandao ya Kijamii, fanyeji kwa weledi – Dkt. Abbas

    April 15, 2021
  • Mkongwe Ali Mayai awapa neno Dodoma Jiji FC

    April 15, 2021
  • Angalia zote

Video

Ni wajibu wa kila mmoja kutambua thamani na nafasi yake katika jamii
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    3 CDA Street

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.